Saturday , 3 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Rais wa madaktari; Mishahara haitukidhi
Habari Mchanganyiko

Rais wa madaktari; Mishahara haitukidhi

Spread the love

RAISI wa Madktari nchini Dk.Elisha Osati, ameiomba serikali kuongeza mishahara kwa watumishi wanaotoa huduma kwenye sekta ya afya nchini ili kumudu mahitaji ya maisha. Anaripoti Faki Sosi, (endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI ONLINE Dk. Elisha Osati amesema kuwa, kwa sasa serikali inatoa mishahara kwa wakati.

“Kwa sasa tunapata mishahara kwa muda muafaka labda kwa waajiriwa wapya ambao pia wanapata mishahara yao kwa muda tu ingawa kunachangamoto ndogondogo,” amesema.

Na kwamba, licha ya mishahara kulipwa kwa wakati  ameeleza kuwa,  bado kiwango cha mishahara hiyo haiendani na namna wanavyoitumikia kada hiyo.

“Kwa kweli mishahara haitoshi hivyo nafikiri ukiongea na daktari yoyete au mafanyakazi yoyete wa sekta ya afya, atakwambia  mishahara haitoshi kwa namna tunavyofanya kazi na muda tunaotumia kutoa huduma za afya,” amesema Dk Osati na kuongeza;

“Bado tunaiomba Serikali  na tunaamini bado inanafasi ya kuongeza mishahara lakini sio serikali tu hata mashirika binafsi hospital, binafsi ambayo kuna madaktari bado tunaomba lipokewe hilo sisi kama  chama cha madakrari tunaangalia weledi wa kitaaluma wa madaktari na huwezi kuzungumzi weledi bila kuzungumzia ustawi wa madaktari”.

Amesema kuwa, amemshukuru Rais John Magofuli na Serikali yake kwa kujali kada hiyo ikiwa pamoja kwa kushughulikia matatizo ya madakri kwa muda muafaka.

Tazama video kamili hapo chini

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Magunia 731 ya bangi yakamatwa, mamia ya hekari yateketezwa Arumeru

Spread the love  MAMIA ya magunia ya madawa ya kulevya aina ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

error: Content is protected !!