Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema, serikali wavutana kuhusu Lissu
Habari za Siasa

Chadema, serikali wavutana kuhusu Lissu

Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeeleza kutishika na matamshi wanayodai kutolewa na mmoja wa mawaziri katika Serikali ya Awamu ya Tano na kwamba, yanatishia usalama wa Tundu Lissu. Anaripoti Faki Sosi… (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 20 Februari 2019 Patrick Ole Sosopi, Mwenyekiti wa Baraza Vijana la Chadema (Bavicha) amesema, matamshi hayo yanazidisha mashaka kuhusu shambulio la Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki.

Sosipi amedai kuwa, kauli ya kutaka kumzamisha Lissu kama mtumbwi baada ya kuponea chupuchupu na kuanza kufanya ziara Ulaya na Marekani huku akiendelea na matibabu nchini Ubelgiji, inaleta taswira hasi.

Lissu ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni alishambuliwa tarehe 7 Septemba 2017 eneo la Area ‘D’ Dodoma.

 Tazama hapa video yote……

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!