Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Deni la taifa lazidi kupaa
Habari za Siasa

Deni la taifa lazidi kupaa

Spread the love

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti imewasilisha taarifa ya mwaka kuhusu utekelezaji wa majukumu yake katika kipindi cha Januari, 2018 hadi Januari 2019 huku ikionesha kuongezeka kwa deni la taifa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Aidha kamati hiyo imebaini kukua kwa deni la taifa likijumuisha fedha zilizokopwa na serikali kutoka katika vyanzo vya ndani na nje pia na sekta binafsi kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo.

Akiwasilisha taarifa ya Kamati ya Bunge leo 2 Februari 2019 bungeni jijini Dodoma, mwenyekiti wa kamati hiyo, George Simbachawene amesema, hadi kufikia Novemba 2018 deni la taifa limeendelea kukua taratibu hadi kufikia Sh 61.8 trilioni.

Pamoja na hayo amesema, ukuaji wa deni hilo umetokana na mahitaji ya uwekezaji kwenye miradi ya maendeleo na kijamii nchini kwa ajili ya kukuza uchumi.

“Kamati inashauri serikali kuangalia uwiano uliopo kati ya mwenendo wa upatikanaji wa mapato ya ndani pamoja na ulipaji wa deni la serikali na athari zake katika bajeti na uchumi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Serikali kuongeza wanufaika mikopo ya elimu ya juu

Spread the loveSERIKALI imesema itaongeza idadi ya wanufaika wa mikopo ya elimu...

ElimuHabari za Siasa

Serikali kufumua mitaala ya vyuo vikuu, ufundi stadi

Spread the loveSERIKALI inakusudia kufanya mapitio katika mitaala na programu za vyuo...

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

error: Content is protected !!