Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Deni la taifa lazidi kupaa
Habari za Siasa

Deni la taifa lazidi kupaa

Spread the love

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti imewasilisha taarifa ya mwaka kuhusu utekelezaji wa majukumu yake katika kipindi cha Januari, 2018 hadi Januari 2019 huku ikionesha kuongezeka kwa deni la taifa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Aidha kamati hiyo imebaini kukua kwa deni la taifa likijumuisha fedha zilizokopwa na serikali kutoka katika vyanzo vya ndani na nje pia na sekta binafsi kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo.

Akiwasilisha taarifa ya Kamati ya Bunge leo 2 Februari 2019 bungeni jijini Dodoma, mwenyekiti wa kamati hiyo, George Simbachawene amesema, hadi kufikia Novemba 2018 deni la taifa limeendelea kukua taratibu hadi kufikia Sh 61.8 trilioni.

Pamoja na hayo amesema, ukuaji wa deni hilo umetokana na mahitaji ya uwekezaji kwenye miradi ya maendeleo na kijamii nchini kwa ajili ya kukuza uchumi.

“Kamati inashauri serikali kuangalia uwiano uliopo kati ya mwenendo wa upatikanaji wa mapato ya ndani pamoja na ulipaji wa deni la serikali na athari zake katika bajeti na uchumi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!