Tuesday , 3 October 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Shilingi ya Tanzania yaporomoka
Habari za Siasa

Shilingi ya Tanzania yaporomoka

Noti za Elfu Kumi
Spread the love

SHILINGI ya Tanzania kwa kipindi kuanzia Julai hadi Novemba 2018 iliporomoka ambapo Dola ya Marekani ilibadilishwa kwa wastani wa Sh. 2,276 ikilinganishwa na Sh. 2,235 katika kipindi cha Julai hadi Novemba mwaka 2017. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Akieleza kuhusu mwenendo wa shilingi ya Tanzania, George Simbachawene, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti amesema, hali hiyo inaonesha shilingi ilipungua thamani dhidi ya Dola ya Marekani kwa asilimia 1.8.

Kamati hiyo imetoa angalizo kwa serikali kuongeza jitihada ya mauzo ya bidhaa na huduma nje.

Licha ya hayo kamati inashauri viwanda vizalishe zaidi bidhaa ambazo zinaagizwa nje kwa wingi kwa kiwa hatua hizi zitasaidia kupunguza nakisi ya urari wa biashara na hivyo kuongeza upatikanaji wa fedha za kigeni na kuongeza thamani ya shilingi.

Mwenyekiti huyo amesema, serikali kwa sasa imelazimika kujielekeza zaidi kukopa mikopo yenye masharti ya kibiashara kuliko yenye mashatyi nafuu kama swali.

Na kwamba, kutokana na ugumu wa upatikanaji wa mikopo hiyo kamati bado inaona mikopo yenye mashari ya kibiashara ina riba kubwa na hivyo kuwepo kwa mzigo mkubwa wa ugharamiaji wa mikopo kupitia mapato ya ndani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

error: Content is protected !!