Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM wajipanga kumrudisha Rais Magufuli 2020
Habari za Siasa

CCM wajipanga kumrudisha Rais Magufuli 2020

Spread the love

MWENYEKITI wa Jumuiya ya wazazi CCM Taifa, Dk. Edmund Mndolwa amewaagiza wajumbe wa Baraza Kuu la Wazazi kujipanga kikamilifu ili wamrudishe madarakani Rais Dk. John Magufuli 2020. Anaripoti Danson Kaijage, kutoka Dodoma … (endelea).

Dk. Mndolwa aliyasema hayo jijini hapa wakati akifunga mkutano wa baraza kuu la wazazi Taifa akisema mwaka 2019 ni mwaka wa ukombozi wa kuhakikisha wanashinda chaguzi zote zijazo.

“Wenzetu wamechoka wako hoi bin taabani na sera zao ni matusi wakilenga kutuzoofisha lakini hawatatuweza lazima tuhakikishe tunawachapa, hata wakijificha uvunguni tuwafuate.

“Huu ni mwaka wa ukombozi kwa CCM kuhakikisha tunashinda uchaguzi wa serikali za mitaa 2019, uchaguzi mkubwa 2020 katika nafasi ya udiwani, ubunge ili kuhakikisha Dk. John Magufuli anarudi madarakani,” alisema Dk Mndolwa.

Baraza hilo pia lilifanya uchaguzi mdogo kuziba nafasi zilizo wazi ambazo ni mjumbe wa halmashauri kuu taifa na mjumbe wa baraza kuu Taifa.

Katibu wa Jumuiya hiyo, Erasto Sima alisema Waliochaguliwa ni Galali Wabanhu mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa akichukua nafasi ya Kitwana Komanya ambaye aliteuliwa kuwa DC wa Tabora na Rajab Mwilima mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa akiziba nafasi ya aliyekuwa mbunge wa Korogwe, Steven Ngonyani ambaye alifariki dunia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!