Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Shabiki apoteza maisha uwanjani
Michezo

Shabiki apoteza maisha uwanjani

Spread the love

SHABIKI wa Inter Milan amepoteza maisha na wengine wanne kujeruhiwa katika mchezo dhidi ya FC Napol uliopigwa kwenye uwanja wa San Siro baada ya kuibuka vurugu kubwa kwa mashabiki wa pande zote mbili kabla ya mechi.

Taarifa kutoka nchini Itaria zinasema kuwa mshabiki huyo alipoteza maisha kwa kugongwa na gari nje ya uwanja kwenye mchezo wa Ligi Kuu uliocheza jana na kushuhudia Inter Milan kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya FC Napol.

Katika mchezo huo ambao uligubikwa na vurugu nyingi ndani na nje ya uwanja kiasi cha kupelekea beki wa kati wa klabu ya Napol anaye windwa na Manchester United, Kalidou Koulibaly kutolewa nje ya uwanja baada ya kuoneshewa kadi mbili za njano.

Licha ya kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa mchezaji huyo, mashabiki wa wa Inter Milan walionekana kufanya vitendo vya ubaguzi wa rangi kwa beki huyo baaada ya kutoa milio kama nyani wakati mchezaji huyo anaposhika mpira uwanjani kiasi kilichompelekea kuandika ujumbe mzito katika ukurasa wake wa mtandao wa Twitter.

Vitendo hivyo ambavyo Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) kuvipinga vikali lakini bado vinaonekana kushamili kwa wachezaji wenye ngozi nyeusi wanaocheza soka la kulipwa barani Afrika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!