Thursday , 9 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Polisi Afrika Kusini wamsaka mke wa Mugabe
Kimataifa

Polisi Afrika Kusini wamsaka mke wa Mugabe

Grace Mugabe, Mke wa Rais wa zamani wa Zambia, Robert Mugabe
Spread the love

MAMLAKA ya Taifa ya Mashtaka nchini Afrika Kusini (NPA) imetoa hati ya kukamatwa kwa Grace Mugabe, mke wa Rais mstaafu wa taifa hilo, Robert Mugabe kuhusiana na tuhuma zinazomkabili za kumshambulia mwanamitindo Gabriella Engels. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Afrika Kusini, Brigedia Vishnu Naidoo amethibitisha kuhusu taarifa hizo akisema kuwa, hati hiyo ilitolewa tarehe 13 Desemba 2018.

Hatua hiyo imekuja baada ya mahakama kumfutia kinga ya kidiplomasia Grace mwezi Julai mwaka huu.

Grace anadaiwa kufanya shambulizi hilo mwaka jana katika hoteli moja ya kifahali inayofahamika kwa jina la Sandton iliyopo mjini Johannesburg, ambapo mwanamitindo huyo anadaiwa alikwenda kuwatembelea vijana wa Mugabe.

Baada ya mwanamitindo huyo kutoa tuhuma hizo, Jeshi la Polisi Afrika Kusini lilimtaka Grace kufika katika kituo cha polisi, lakini hakutokea licha ya awali kuahidi kwamba angeitikia wito. Na kurejea nchini kwake Zimbabwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!