Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Polisi Afrika Kusini wamsaka mke wa Mugabe
Kimataifa

Polisi Afrika Kusini wamsaka mke wa Mugabe

Grace Mugabe, Mke wa Rais wa zamani wa Zambia, Robert Mugabe
Spread the love

MAMLAKA ya Taifa ya Mashtaka nchini Afrika Kusini (NPA) imetoa hati ya kukamatwa kwa Grace Mugabe, mke wa Rais mstaafu wa taifa hilo, Robert Mugabe kuhusiana na tuhuma zinazomkabili za kumshambulia mwanamitindo Gabriella Engels. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Afrika Kusini, Brigedia Vishnu Naidoo amethibitisha kuhusu taarifa hizo akisema kuwa, hati hiyo ilitolewa tarehe 13 Desemba 2018.

Hatua hiyo imekuja baada ya mahakama kumfutia kinga ya kidiplomasia Grace mwezi Julai mwaka huu.

Grace anadaiwa kufanya shambulizi hilo mwaka jana katika hoteli moja ya kifahali inayofahamika kwa jina la Sandton iliyopo mjini Johannesburg, ambapo mwanamitindo huyo anadaiwa alikwenda kuwatembelea vijana wa Mugabe.

Baada ya mwanamitindo huyo kutoa tuhuma hizo, Jeshi la Polisi Afrika Kusini lilimtaka Grace kufika katika kituo cha polisi, lakini hakutokea licha ya awali kuahidi kwamba angeitikia wito. Na kurejea nchini kwake Zimbabwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Wadukuzi wa Kichana waiba barua pepe 60,000 za Serikali ya Marekani

Spread the loveWADUKUZI wa kichana wamedukua barua pepe 60000 serikali ya Marekani...

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

error: Content is protected !!