Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Upelelezi wakwamisha kesi ya Wema
Habari za Siasa

Upelelezi wakwamisha kesi ya Wema

Wema Sepetu (kulia) akitoka na mama yake mahakamani Kisutu
Spread the love

KESI ya kuchapisha na kusambaza video ya ngono inayomkabili msanii wa filamu nchini, Wema Sepetu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirishwa hadi tarehe 12 Desemba 2018, kutokana na upande wa mashtaka kutokamilisha upelelezi. Anaripoti mwandishi Wetu … (endelea).

Kesi hiyo iliyofunguliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) dhidi ya Wema, leo tarehe 21 Novemba 2018 ilitakiwa kutajwa tarehe, lakini imeahirishwa kutokana na upande wa mashtaka kutokamilisha upelelezi wa kesi hiyo.

Hakimu anayesimamia kesi hiyo, Hakimu Maira Kasonde aliiahirisha kesi hiyo. Upande wa jamhuri unasimamiwa na Wakili Jenifer Masue huku wakili wa utetezi akiwa Ruben Simwanza.

Mnamo tarehe mosi Novemba 2018 Wema alipandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ikiwa siku kadhaa zimepita tangu aliposambaza mitandaoni video yake inayomuonyesha akiwa faragha na mpenzi wake anayefahamika kwa jina la PCK.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!