Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Upelelezi wakwamisha kesi ya Wema
Habari za Siasa

Upelelezi wakwamisha kesi ya Wema

Wema Sepetu (kulia) akitoka na mama yake mahakamani Kisutu
Spread the love

KESI ya kuchapisha na kusambaza video ya ngono inayomkabili msanii wa filamu nchini, Wema Sepetu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirishwa hadi tarehe 12 Desemba 2018, kutokana na upande wa mashtaka kutokamilisha upelelezi. Anaripoti mwandishi Wetu … (endelea).

Kesi hiyo iliyofunguliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) dhidi ya Wema, leo tarehe 21 Novemba 2018 ilitakiwa kutajwa tarehe, lakini imeahirishwa kutokana na upande wa mashtaka kutokamilisha upelelezi wa kesi hiyo.

Hakimu anayesimamia kesi hiyo, Hakimu Maira Kasonde aliiahirisha kesi hiyo. Upande wa jamhuri unasimamiwa na Wakili Jenifer Masue huku wakili wa utetezi akiwa Ruben Simwanza.

Mnamo tarehe mosi Novemba 2018 Wema alipandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ikiwa siku kadhaa zimepita tangu aliposambaza mitandaoni video yake inayomuonyesha akiwa faragha na mpenzi wake anayefahamika kwa jina la PCK.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!