Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kisukari, Saratani yapunguziwe mzigo wa matibabu
Habari za Siasa

Kisukari, Saratani yapunguziwe mzigo wa matibabu

Hospitali ya magonjwa ya Kansa ya Ocean Road
Spread the love

MBUNGE wa Viti Maalum (CUF), Rukia Ahmed ameitaka serikali kuwaondolewa ukali wa gharama za matibabu, waathirika wa magonjwa yasiyo ya kuambukiza hasa kisukari na saratani. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Rukia ametoa wito huo wakati akiuliza swali kwa Wizara ya Afya, akisema kuwa magonjwa yasiyo ya kuambukiza, ikiwemo kisukari na saratani matibabu yake yamekuwa ghali na hayako ya moja kwa moja, na kuitaka serikali kutoa msimamo wake katika kuboresha huduma ya waathirika wa magonjwa haya hususan kwenye matibabu.

Akijibu swali hilo kwa niaba ya Waziri wa Afya, Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamis Kigwangalla amesema serikali inaendelea kuhimiza wananchi hasa waathirika wa magonjwa yasiyo ya kuambukiza kujiunga na bima ya afya ili kupunguza mzigo wa gharama za matibabu.

“Gharama za magonjwa yasiyo ya kuambikiza ni kubwa mno, serikali imeanzisha mkakati wa kuhamasisha watu kuishi maisha ya afya, kuangalia vyakula wanavyokula, kufanya mazoezi, hivyo ili kuepuka gharama za kutibu . Tunaendelea kuhamasisha zaidi kinga kuliko tiba, kuna mkakati watu wote wawe na bima ya afya ili huo mzigo wa gharama usiweze kuwa mkubwa na badala yake ubebwe na jamii,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!