Monday , 29 May 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Kuanguka Trump, mwanasheria mkuu ang’oka
Kimataifa

Kuanguka Trump, mwanasheria mkuu ang’oka

Spread the love
MWANASHERIA Mkuu wa Marekani, Jeff Sessions amejiuzulu wadhifa huo akitekeleza agizo la Rais Donald Trump, lililomtaka kuachia ngazi. Yanaripoti Mashirika ya Kimataifa …(endelea).
Trump alitoa agizo hilo jana tarehe 7 Novemba 2018, ikiwa ni masaa 24 baada ya chama chake cha Republican kupoteza udhibiti wake katika Bunge la Wawakilishi, kufuatia kuanguka katika uchaguzi wa kati kati ya muhula uliofanyika juzi Jumanne.
Katika barua yake ya kujiuzulu aliyoiwasilisha hapo jana, Sessions aliandika kwamba uamuzi wake wa kujiuzulu unatokana na agizo la Trump, lililomtaka kujiuzulu.
Kupitia akaunti yake ya Twitter, Trump alimpongeza Sessions kwa hatua yake ya kujiuzulu na utumishi wake wakati akiwa Mwanasheria Mkuu.
Katika hatua nyingine, Trump amemteua Matthew Whitaker kukaimu nafasi ya Mwanasheria Mkuu hadi pale atakapoteuliwa mtu kushikiliwa wadhifa huo.
Awali Trump alikuwa amekosana na Whitaker kutokana na kutofurahishwa kwake na hatua ya kujiondoa katika uchunguzi wa FBI kuhusu madai ya Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani 2016. Alidai kuwa Sessions alikuwa na msimamo dhaifu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mkutano wa Quad Hiroshima waibuka na kutafuta amani na ustawi wa Indo-Pacific

Spread the love  JITIHADA za mazungumzo ya Pande Nne (Quad), hazikuthaminiwa na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Kimataifa

Kiwango cha ukosefu wa ajira nchini China chaongezeka

Spread the love  WAKATI kiwango cha ukosefu wa ajira kwa vijana nchini...

Kimataifa

Kampuni za kigeni zahofia kuendelea na biashara China

Spread the love OPERESHENI ya kiuchunguzi inayofanywa na Serikali ya China kwa...

error: Content is protected !!