SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amegoma kuruhusu swali la Mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe kutolewa majibu na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, swali hilo lilihusu sakata la Balozi wa Jumuiya ya Ulaya (EU), Roeland Van de Geer kuitwa kwao. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Hivi karibuni Balozi, Van de Geer aliitwa makao makuu ya EU yaliyoko mjini Brussels nchini Ubelgiji kwa kile kilichoelezwa kuwa, kwenda kujadili masuala ya kisiasa na uhusiano baina ya Tanzania na jumuiya hiyo.
Wakati akiuliza swali kwa Waziri Mkuu, leo tarehe 8 Novemba 2018 bungeni jijini Dodoma, Mwambe alitaka kujua msimamo wa serikali kuhusu madai ya kudorola kwa mahusiano mazuri baina ya Tanzania na EU kufuatia hatua ya jumuiya hiyo kumuondoa balozi wake..
Lakini, Spika Ndugai alimzuia Waziri Mkuu kujibu swali hilo, akieleza kuwa maelezo ya swali hilo yanampa tabu kuruhusu swali hilo.
“Napata tabu kuruhu ili swali, maelezo yako unasema aliitwa huko kwao, sasa unataka waziri Mkuu ajibu nini?
Leave a comment