Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sakata la Balozi wa EU latinga bungeni, Spika aligomea
Habari za SiasaTangulizi

Sakata la Balozi wa EU latinga bungeni, Spika aligomea

Spread the love

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amegoma kuruhusu swali la Mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe kutolewa majibu na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, swali hilo lilihusu sakata la Balozi wa Jumuiya ya Ulaya (EU), Roeland Van de Geer kuitwa kwao. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Hivi karibuni Balozi, Van de Geer aliitwa makao makuu ya EU yaliyoko mjini Brussels nchini Ubelgiji kwa kile kilichoelezwa kuwa, kwenda kujadili masuala ya kisiasa na uhusiano baina ya Tanzania na jumuiya hiyo.

Wakati akiuliza swali kwa Waziri Mkuu, leo tarehe 8 Novemba 2018 bungeni jijini Dodoma, Mwambe alitaka kujua msimamo wa serikali kuhusu madai ya kudorola kwa mahusiano mazuri baina ya Tanzania na EU kufuatia hatua ya jumuiya hiyo kumuondoa balozi wake..

Lakini, Spika Ndugai alimzuia Waziri Mkuu kujibu swali hilo, akieleza kuwa maelezo ya swali hilo yanampa tabu kuruhusu swali hilo.

“Napata tabu kuruhu ili swali, maelezo yako unasema aliitwa huko kwao, sasa unataka waziri Mkuu ajibu nini?

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!