Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ukawa waanza kwa kususa bungeni
Habari za SiasaTangulizi

Ukawa waanza kwa kususa bungeni

Spread the love

UMOJA wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) bungeni wamesusa kushuhudia kuapishwa kwa wabunge wanne. Anaandika Dany Tibason, Dodoma … (endelea).

Leo vikao vya bunge vimeanza Jijini Dodoma ambapo baada ya dua ya ufunguzi, tukio lililofuata lilikua la kuapishwa kwa wabunge hao.

Wabunge hao ambao awali walikuwa upinzani ni Julius Kalanga (Monduli), Timotheo Mzava (Korogwe vijijini), Mwita Waitara (Ukonga) na Zuberi Kuchauka (Liwale).

Wabunge wa CUF kambi ya Prof. Ibrahim Lipumba walisalia ndani ya ukumbi wa bunge wakati wa tukio hilo.

Kelele na vigelegele vilisikika wakati wapinzani wakitoka bungeni ambapo baadhi ya wabunge wa CCM walikwenda kukaa upande wa viti vya upinzani.

Baada ya wabunge hao kuapishwa, wapinzani walirejea bungeni kuendelea na ratiba ya siku.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

error: Content is protected !!