Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ukawa waanza kwa kususa bungeni
Habari za SiasaTangulizi

Ukawa waanza kwa kususa bungeni

Spread the love

UMOJA wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) bungeni wamesusa kushuhudia kuapishwa kwa wabunge wanne. Anaandika Dany Tibason, Dodoma … (endelea).

Leo vikao vya bunge vimeanza Jijini Dodoma ambapo baada ya dua ya ufunguzi, tukio lililofuata lilikua la kuapishwa kwa wabunge hao.

Wabunge hao ambao awali walikuwa upinzani ni Julius Kalanga (Monduli), Timotheo Mzava (Korogwe vijijini), Mwita Waitara (Ukonga) na Zuberi Kuchauka (Liwale).

Wabunge wa CUF kambi ya Prof. Ibrahim Lipumba walisalia ndani ya ukumbi wa bunge wakati wa tukio hilo.

Kelele na vigelegele vilisikika wakati wapinzani wakitoka bungeni ambapo baadhi ya wabunge wa CCM walikwenda kukaa upande wa viti vya upinzani.

Baada ya wabunge hao kuapishwa, wapinzani walirejea bungeni kuendelea na ratiba ya siku.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!