Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri Mkuu astukia ufisadi Dodoma
Habari Mchanganyiko

Waziri Mkuu astukia ufisadi Dodoma

Spread the love

KASSIM Majaliwa, Waziri Mkuu amestukia ufisadi wa Sh. 1.2 bilioni  katika sekta ya kilimo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akiwa kwenye ziara  yake wilayani Chamwino, Dodoma Majaliwa amepokea taarifa ya ubadhirifu wa fedha hizo zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya mradi wa umwagiliaji ambazo matumizi yake hayajulikani

Akizungumza na wananchi wa Tarafa ya Mpwayungu, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Mpwayungu amemuagiza Dk. Bilinith Mahenge, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amuagize Ofisa Kilimo wa Mkoa huo Bernad Abraham kwenda kwenye mradi huo kwa ajili ya ukaguzi ili kubaini wezi wa pesa hizo.

Wakati huo huo  Waziri Mkuu alivunja kamati ya kusimamia huduma maji ya kijiji cha Mpwayungu na alimuagiza Mhandisi wa Maji wa wilaya ya Chamwino, Godfrey Mbabaye aunde kamati mpya.

Waziri Mkuu alichukua hatua hiyo baada ya kutoridhishwa na utendaji wa kamati hiyo ambayo ilishindwa kutekeleza majukumu yake ikiwemo ujenzi wa vituo vya kuchotea maji licha ya kukusanya Sh. 20 milioni kwa mwezi, mradi huo unavituo vinne tu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!