Thursday , 18 April 2024
Home Kitengo Michezo Ammy Ninje Mkurugenzi wa Ufundi TFF
Michezo

Ammy Ninje Mkurugenzi wa Ufundi TFF

Ammy Ninje, Mkurugenzi wa Ufundi TFF
Spread the love

KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imemteuwa kocha Ammy Ninje kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Ufundi ndani ya shirikisho hilo leo Oktoba 22, 2018, na awali nafasi hiyo ilikuwa inashikiliwa na Oscar Milambo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Ammy Ninje alishawahi kuiongoza timu ya Taifa ya Tanzania Bara Kilimanjaro Stars kwenye michuano ya CECAFA iliofanyika nchini Kenya mwaka uliopita na kuwahi kuwa kocha wa timu ya Taifa ya Tanzania chini ya umri wa miaka 20, ‘Ngorongoro Heroes.’

Bada ya kuondolewa katika nafasi hiyo Oscar Milambo ataendelea na majukumu yake kama Ofisa Maendeleo wa Vijana ndani ya shirikisho hilo na wakati huo huo kamati ya utendaji imepitisha tarehe ya mkutano mkuu ambao kisheria unatakiwa kutangazwa siku 60 kabla ya kufanyika.

Aidha kikao hicho cha Kamati ya Utendaji kimefanya mabadiliko kwenye baadhi ya kamati kutokana na baadhi ya Wajumbe kujiuzulu na wengine kukabiliwa na majukumu mengi.

Wajumbe walioteuliwa kwenye Kamati ya Nidhamu ni Kiomoni  Kibamba ambaye ni  Mwenyekiti huku wajumbe ni Peter Hella, Kassim Dau, Handley Matwenga na Twaha Mtengera. Huku Kamati ya Rufaa na Maadili itaongozwa na Richard Mbaruku ambaye ni Mwenyekiti, Makamo wake, Thadeus Karua  wajumbe ni Mussa Zungu, ASP Benedict Nyagabona na Lugano Hosea.

Kwa upande wa Kamati ya Uchaguzi wataongozwa na Mwenyekiti, Malangwe Ally huku Makamo wake akiwa Mohamed Mchengela, Benjamini Karume, Mohamed Gombati, Hamisi Zayumba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!