Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Manara achomoka sakata la MO
Habari Mchanganyiko

Manara achomoka sakata la MO

Haji Manara
Spread the love

MKUU wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Haji Manara pamoja na watu 19 waliokuwa wanashikiliwa kutokana na sakata la kutekwa kwa Mfanyabishara Mohammed Dewji ‘Mo Dewji’,  wamechwa huru kwa dhamana. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa inaeleza kuwa Manara na wenzake wameachwa kwa dhamana usiku wa jana tarehe 15 Oktoba 2018.

Manara aliyesota rumande tangu Oktoba 12 mwaka huu hadi usiku wa jana, alikamatwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kusambaza taarifa za tukio la kutekwa kwa Mo Dewji akidai alitumwa na familia ya mfanyabiashara huyo, wakati si kweli.

Katika sakata hilo, watu 7 kati ya 26 akiwemo Manara na wenzake 19 walioachwa huru kwa dhamana, bado wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam wakihusishwa na tukio la Kutekwa kwa Mo Dewji lilitokea katika hoteli ya Colosseum jijini Dar es Salaam Oktoba 11 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!