TUME ya Uchaguzi Tanzania (NEC) imetangaza tarehe ya Uchaguzi wa Marudio katika majimbo ya Serengeti na Simanjiro utakaofanyika tarehe 2 Desemba, 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Uchaguzi huo utafanyika baada ya kujiuzuru kwa wabunge wake, James Ole Millya wa Simanjiro na Marwa Chacha wa Serengeti, ikiwa pamoja na Kata 21 za Tanzania Bara ambapo pia madiwani wake wamejiuzuru.
Mwenyekiti wa NEC,Semistocles Kaijage amesema fomu za uteuzi wa wagombea zitatolewa tarehe 28 Oktoba hadi 3 Novemba mwaka huu.
Leave a comment