Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Familia ya Dewji kutoa bil 1 kwa atakayesaidia kupatikana MO
Habari MchanganyikoTangulizi

Familia ya Dewji kutoa bil 1 kwa atakayesaidia kupatikana MO

Spread the love

FAMILIA ya Mfanyabiashara, Mohammed Dewji ‘MO’ aliyetekwa tangu Alhamisi ya Oktoka 11 2018, maeneo ya Osterbay jijini Dar es Salaam, imetangaza zawadi nono ya kiasi cha Sh. 1 bilioni, kwa mtu atakayetoa taarifa zitakazowezesha kupatikana kwa mfanyabiashara huyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Zawadi hiyo imetangazwa leo tarehe 15 Oktoba 2018 jijini Dar es Salaam na Msemaji wa Familia ya Gullam Dewji, Azim Dewji wakati akizungumza na wanahabari.

“Familia ya Mzee Gulam inasikitika kutangaza kutekwa kwa mtoto wao mpendwa MO, mtendaji mkuu wa METL. Aidha, tunapenda kuishukuru serikali kwa jitihada kubwa wanazofanya kuhakikisha tunampata mtoto wetu, vile vile tunavishukuru vyombo vya habariokwa kazi kubwa, taasisi za dini na zisizo za dini kwa maombi na kutufariji katika kipindi hiki tunaomba muendelee,” amesema.

“Katika kuongeza juhudi za kuhakikisha mtoto wetu mpendwa anapatikana, familia inapenda kutangaza zwadi nono ya fedha za kitanzania bilioni 1 kwa yeyote atakayetoa taarifa muhimu zitakazopelekea kupatikana kwa Mo,” amesema msemaji huyo wa familia ya Dewji.

Azzim ameeleza kuwa, familia hiyo itatunza siri za mtu atakaye toa taarifa za kupatikana kwa Mo Dewji, huku akitaja mawasiliano ya familia hiyo kwa mtu atakayetaka kutoa taarifa.

“Familia inaahidi kutunza taarifa kwa siri kubwa ya mtoa taarifa. Kwa yeyote mwenye taarifa aitoe kwenye namba 0755030014, au 0717208478 na 0784783228,” amesema Azim.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

error: Content is protected !!