Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Serikali yanunua mashine 10 za X-ray
Afya

Serikali yanunua mashine 10 za X-ray

Spread the love

MASHINE kumi za mionzi (digital X-ray) zenye thamani ya Sh. 1.74 bilioni zimenunuliwa na serikali kwa ajili ya kuboresha huduma za afya nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mashine hizo zimepokelewa leo tarehe 2 Oktoba 2018 na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu kutoka katika Bohari ya Dawa (MSD) jijini Dar es Salaam.

Baada ya kupokea mashine hizo, Waziri Ummy amesema mashine hizo zitapelekwa kwenye hospitali za rufaa za mikoa 10 ambazo baadhi yake X-ray zilizokuwepo zimekwisha muda wake.

Hospitali hizo ni pamoja na Amana, Bukoba, Katavi, Morogoro, Njombe, Ruvuma, Simiyu na Singida pamoja na hospitali za Wilaya ya Magu na Nzega.

“Maendeleo ya Taifa letu la Tanzania yataletwa na wananchi wenye afya na wenye uwezo wa kuzalisha mali,hivyo tunaboresha na kuimarisha huduma za tiba na uchunguzi wa magonjwa katika hospitali zetu kuwa na vifaa vya kisasa zaidi na kuondokana na utaratibu wa kupeleka wagonjwa nje ya nchi,” amesema Waziri Mwalimu.

Waziri Ummy amesema Serikaki inaendelea kutoa kipaumbele katika kuboresha huduma za afya nchini ikiwa ni lengo la kuhakikisha huduma za afya zinawafikia watanzainia wote karibu na maeneo wanayoishi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

error: Content is protected !!