Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko WhatsApp ilivyotumika kuvujisha mtihani
Habari Mchanganyiko

WhatsApp ilivyotumika kuvujisha mtihani

Whatsapp
Spread the love

BARAZA la Mitihani la Taifa (NECTA) limewasimamisha kazi maafisa elimu, maafisa taaluma, waratibu wa elimu na wakuu wa shule za msingi  wa Wilaya ya Chemba na Kondoa kwa tuhuma za kuvujisha mtihani wa kumaliza elimu ya msingi wa mwaka 2018 uliofanyika Septemba 5 hadi 6 mwaka huu. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji NECTA, Dk. Charles Msonde amedai kuwa, watuhumiwa hao kwa makusudi walifanya udanganyifu wa mtihani huo kwa kuunda kundi la siri la Whatsapp ambalo walilitumia kusambaza mtihani huo kwa lengo la kupandisha ufaulu wa shule za Halmahsuri ya Chemba .

Akieleze kuhusu tukio hilo, Dk. Msonde amedai kuwa, uongozi wa elimu Halmashauri ya Chemba kwa kushirikiana na waratibu wa elimu kata na wakuu wa shule waliufungua mtihani huo siku moja kabla ya terehe iliyopangwa kufanyika, ambapo waalimu hao walifanya kazi ya kukokotoa majibu yake kisha kusambaza kwa wakuu wa shule ambao walifikisha majibu hayo kwa watahiniwa.

“Tukio la halmashauri ya Chemba mkoani Dodoma, uongozi wa idara ya elimu  wa halmashauri hiyo ulipanga kwa makusudi kufanya udanganyifu wa mitihani hii ya kumaliza elimu ya msingi, viongozi walipanga kwa kushirikiana na waratibu wa elimu kata na wakuu wa shule, na ili kufanikisha azma hiyo, kamati ya mitihani ya mkoa wa Dodoma pamoja na uchunguzi wa NACTE ulibaini pasina shaka waliunda makundi ya whatsap yaliyowashirikisha uongozi wa elimu na waratinu wa elimu wakayafunga kwa siri ili wawe na mawasiliano miongoni mwao ya uhakika na haraka,” amesema na kuongeza.

“Mtihani ulipofika kwao siku moja kabla ya mtihani kufanyika tarehe 4 Septemba 2018  mitihani ilifunguliwa na kusambazwa katika makundi hayo, kwa minajili ya kukokotolewa na kupatiwa majawabu na kuwafikishia wakuu wa shule ili wapewe watahiniwa na kupandisha ufaulu wa halmashauri yao.Viongozi hawa walikuwa wakitoa maelekezo kwa waratibu namna ya kutekeleza waliyopanga waweze kufanikisha azma hiyo.”

Dk. Msonde aliwataja vinara wa mpango huo, akiwemo Kaimu Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Chemba, Modest Tarimo akisaidiwa kwa karibu na Afisa Taaluma wa Elimu Msingi wa halmshauri hiyo, Ally Akida pamoja na kiongozi aliyepewa jukumu la kutunza makundi ya whatsap ambaye ni Mratibu wa Elimu Kata wa Farkwa, Deo Phillip alishirikiana na baadhi ya wakuu wa shule.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Ditopile aungana na Wana-Kongwa kwa Iftar, wamuombea dua Rais Samia

Spread the loveKATIKA muendelezo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Mbunge wa Viti...

Habari Mchanganyiko

PSSSF yawekeza kwenye viwanda 4, kuzalisha ajira 3,000

Spread the loveKATIKA kuisaidia Serikali kupunguza tatizo la uhaba wa ajira nchini,...

Habari Mchanganyiko

Luhemeja ahimiza utunzaji rasilimali maji kwa faida ya vizazi vijavyo

Spread the love  NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Cyprian Luhemeja...

Habari Mchanganyiko

NSSF yawapa darasa wahariri uwekezaji wa nyumba, yapewa cheti

Spread the loveMFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umetoa wito...

error: Content is protected !!