Sunday , 5 May 2024
Home Kitengo Michezo Anthony Joshua aendeleza rekodi ya kibabe
Michezo

Anthony Joshua aendeleza rekodi ya kibabe

Spread the love

BONDIA wa Uingereza, Anthony Joshua (28), usiku wa kuamkia Jumapili Septemba 23, 2018, ameendeleza ubabe kwa kumtwanga Alexander Povetkin (39) kwa KO (Knock Out) katika raundi ya saba. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mpambano huo wa uzito wa juu wa raundi 12 uliochezwa nchini Uingereza, uliwakutanisha wababe hao wenye rekodi nzuri za ushindi ambapo kabla ya mchezo huo, Joshua alikuwa na rekodi ya kucheza michezo 21 bila kupoteza wakati Povetkin akicheza michezo 37 na kupoteza mmoja.

Mpambano huo uliohudhuriwa na watazamaji 80,000 ulimshuhudia Povetkin maarufu kama Simba Mweupe, akianza mchezo kwa kasi na kufanikiwa kumchana pua ya Joshua katika raundi ya pili baada ya kumshushia konde zito.

Joshua mwenye asili ya Nigeria alicharuka na kufanikiwa kumuangusha mara mbili mpinzani wake kabla ya mwamuzi kukatisha pambano kwenye mzunguko wa saba ili kunusuru uhai wa Povetkin.

Kwa ushindi huo, Joshua amefanikiwa kujiingizia kitita cha Pauni za Uingereza 20 milioni (sawa na Sh. 59.6 bilioni) huku mpinzani wake akiingiza pauni 6 milioni (sawa na Sh. 17.8 bilioni).

Joshua ambaye Mama yake ni Mwafrika kutoka nchini Nigeria ameendelea kushikilia mikanda yake mitatu ya Uzito wa juu inayotambulika na WBC, WBA na IBF.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

error: Content is protected !!