Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwita Waitara arudi tena Ukonga
Habari za Siasa

Mwita Waitara arudi tena Ukonga

Mwita Waitara, Naibu wa Waziri wa TAMISEMI
Spread the love

MGOMBEA Ubunge wa CCM katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Ukonga uliofanyika jana, Mwita Waitara ameibuka mshindi baada ya kupata kura ya asilimia 89.1. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Waitara ametangazwa mshindi leo tarehe 17 Septemba 2018 na Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Ukonga, Jumanne Shauri, ambapo msimamizi huyo alisema Waitara alipata kura 77,795.

Katika uchaguzi huo, mpinzani wa karibu alikuwa mgombea wa Chadema, Asia Msangi aliyeambulia kura 8,676 sawa na asilimia 9.95.

Wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Shauri alisema waliopiga kura ni asilimia 29.4 kati ya watu 300,609 ya waliotarajiwa kupiga kura.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!