MGOMBEA Ubunge wa CCM katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Ukonga uliofanyika jana, Mwita Waitara ameibuka mshindi baada ya kupata kura ya asilimia 89.1. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Waitara ametangazwa mshindi leo tarehe 17 Septemba 2018 na Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Ukonga, Jumanne Shauri, ambapo msimamizi huyo alisema Waitara alipata kura 77,795.
Katika uchaguzi huo, mpinzani wa karibu alikuwa mgombea wa Chadema, Asia Msangi aliyeambulia kura 8,676 sawa na asilimia 9.95.
Wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Shauri alisema waliopiga kura ni asilimia 29.4 kati ya watu 300,609 ya waliotarajiwa kupiga kura.
Leave a comment