Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Bobi Wine alazwa ICU, madaktari wasema alipewa sumu
KimataifaTangulizi

Bobi Wine alazwa ICU, madaktari wasema alipewa sumu

Spread the love

MBUNGE wa Kyadondo Mashariki nchini Uganda, Robert Kyagulanyi hali yake kiafya ni tete, amelazwa katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU) nchini Marekani alikokwenda kupatiwa matibabu. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa kutoka kwa madaktari wanaomuuguza Kyagulanyi ambaye kwa jina maarufu anafahamika kama ‘Bobi Wine’, zianeleza kuwa mwanasiasa huyo yuko katika uangalizi maalumu kutokana na ogani zake za ndani kuharibika.

Kuharibika kwa ogani za ndani za Bobi Wine  kumemsababishia  mwanasiasa huyo kupata tatizo la damu kuvuja ndani kwa ndani, na kwenye matundu ya pua na masikio.

Vile vile, taarifa hiyo inaeleza kuwa, Bobi Wine alipokuwa kizuizini alichomwa sindano yenye sumu.

Bobi Wine amepata matatizo ya kiafya baada ya kuwekwa kizuini hivi karibuni, ambapo inadaiwa aliteswa na kupigwa na maafisa wa usalama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

error: Content is protected !!