Friday , 2 June 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Bobi Wine alazwa ICU, madaktari wasema alipewa sumu
KimataifaTangulizi

Bobi Wine alazwa ICU, madaktari wasema alipewa sumu

Spread the love

MBUNGE wa Kyadondo Mashariki nchini Uganda, Robert Kyagulanyi hali yake kiafya ni tete, amelazwa katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU) nchini Marekani alikokwenda kupatiwa matibabu. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa kutoka kwa madaktari wanaomuuguza Kyagulanyi ambaye kwa jina maarufu anafahamika kama ‘Bobi Wine’, zianeleza kuwa mwanasiasa huyo yuko katika uangalizi maalumu kutokana na ogani zake za ndani kuharibika.

Kuharibika kwa ogani za ndani za Bobi Wine  kumemsababishia  mwanasiasa huyo kupata tatizo la damu kuvuja ndani kwa ndani, na kwenye matundu ya pua na masikio.

Vile vile, taarifa hiyo inaeleza kuwa, Bobi Wine alipokuwa kizuizini alichomwa sindano yenye sumu.

Bobi Wine amepata matatizo ya kiafya baada ya kuwekwa kizuini hivi karibuni, ambapo inadaiwa aliteswa na kupigwa na maafisa wa usalama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Kimataifa

Kauli ya Rais wa China kuhusu ajira yawakatisha tamaa vijana

Spread the love  KAULI ya hivi karibuni ya Rais wa China, Xi...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

error: Content is protected !!