Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Bobi Wine alazwa ICU, madaktari wasema alipewa sumu
KimataifaTangulizi

Bobi Wine alazwa ICU, madaktari wasema alipewa sumu

Spread the love

MBUNGE wa Kyadondo Mashariki nchini Uganda, Robert Kyagulanyi hali yake kiafya ni tete, amelazwa katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU) nchini Marekani alikokwenda kupatiwa matibabu. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa kutoka kwa madaktari wanaomuuguza Kyagulanyi ambaye kwa jina maarufu anafahamika kama ‘Bobi Wine’, zianeleza kuwa mwanasiasa huyo yuko katika uangalizi maalumu kutokana na ogani zake za ndani kuharibika.

Kuharibika kwa ogani za ndani za Bobi Wine  kumemsababishia  mwanasiasa huyo kupata tatizo la damu kuvuja ndani kwa ndani, na kwenye matundu ya pua na masikio.

Vile vile, taarifa hiyo inaeleza kuwa, Bobi Wine alipokuwa kizuizini alichomwa sindano yenye sumu.

Bobi Wine amepata matatizo ya kiafya baada ya kuwekwa kizuini hivi karibuni, ambapo inadaiwa aliteswa na kupigwa na maafisa wa usalama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!