Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Michezo Mbeya City yaendelea kupata tabu Ligi Kuu
Michezo

Mbeya City yaendelea kupata tabu Ligi Kuu

Spread the love

TIMU ya Mbeya City imeendelea kupata tabu katika Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya kupoteza mchezo wa tatu mfululizo dhidi ya Mtibwa Sugar kwa mabao 2-1, mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Mbeya City ilianza kwa kichapo katika mchezo wao dhidi ya Simba mabao 2-0 kabla kupigwa tena idadi kama hiyo na klabu ya Azam FC. 

Mabao ya Mtibwa katika mchezo wa leo yalifungwa na Stamili Mbonde katika dakika ya tisa, Ismail Mhesa 42 na bao pekee la kufutia machozi kwa Mbeya City lilifungwa na Eric Kyaruzi.

Kwa matokeo hayo Mbeya City itakuwa imeruhusu jumla ya mabao sita mpaka sasa katika michezo mitatu iliyocheza na kuendelea kuburuza mkia katika msimamo wa ligi kuu Tanzania bara na kufanya kuwa na mwanzo mbaya.

Licha ya kutokuwa na nyota wao wawili muhimu wa kikosi cha kwanza Kelvin Sabato na Salum Kihimbwa ambao wapo kwenye majukumu ya timu ya Taifa, Mtibwa ilionekana kucheza vizuri na kumiliki mpira muda wote wa mchezo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

error: Content is protected !!