Sunday , 3 December 2023
Home Kitengo Michezo Mbeya City yaendelea kupata tabu Ligi Kuu
Michezo

Mbeya City yaendelea kupata tabu Ligi Kuu

Spread the love

TIMU ya Mbeya City imeendelea kupata tabu katika Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya kupoteza mchezo wa tatu mfululizo dhidi ya Mtibwa Sugar kwa mabao 2-1, mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Mbeya City ilianza kwa kichapo katika mchezo wao dhidi ya Simba mabao 2-0 kabla kupigwa tena idadi kama hiyo na klabu ya Azam FC. 

Mabao ya Mtibwa katika mchezo wa leo yalifungwa na Stamili Mbonde katika dakika ya tisa, Ismail Mhesa 42 na bao pekee la kufutia machozi kwa Mbeya City lilifungwa na Eric Kyaruzi.

Kwa matokeo hayo Mbeya City itakuwa imeruhusu jumla ya mabao sita mpaka sasa katika michezo mitatu iliyocheza na kuendelea kuburuza mkia katika msimamo wa ligi kuu Tanzania bara na kufanya kuwa na mwanzo mbaya.

Licha ya kutokuwa na nyota wao wawili muhimu wa kikosi cha kwanza Kelvin Sabato na Salum Kihimbwa ambao wapo kwenye majukumu ya timu ya Taifa, Mtibwa ilionekana kucheza vizuri na kumiliki mpira muda wote wa mchezo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Manchester City dhidi ya Tottenham ni usiku wa kisasi

Spread the love KIPUTE kati ya klabu ya Manchester City dhidi yaTottenham Hotspurs...

Michezo

Wikiendi ya kutamba na Meridianbet hii hapa usikubali kuikosa

Spread the loveMERIDIANBET wanakwenda kukupa nafasi ya kutambawikiendi hii kupitia ODDS KUBWA walizoweka...

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

Michezo

Meridianbet na Ligi ya Europa inakupa pesa za kumwaga mapema sana

Spread the love  KOMBE la UEFA Europa League ni zito kuliko makombe...

error: Content is protected !!