Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Katibu wa Bunge aficha sababu za Ghasia kujiuzuru
Habari za Siasa

Katibu wa Bunge aficha sababu za Ghasia kujiuzuru

Spread the love

HAWA Ghasia, Mbunge wa Mtwara Vijijini kupitia CCM, amejiuzulu uenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti leo tarehe 28 Agosti, 2018. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Vilevile, Jitu Soni, Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo pia amejiuzulu wadhifa huo.

Taarifa hizo zimethibitishwa na Stephen Kagaigai, Katibu wa Bunge alipozungumza na mtandao huu kwa njia ya simu.

Hata hivyo, Kagaigai hakutaka kuzungumzia sababu zilizopelekea viongozi hao kujiuzulu zaidi ya kusema kwamba Bunge lina taarifa za kujiuzulu kwao.

MwanaHALISI Online ilimtafuta Hawa Ghasia kwa njia ya simu kwa ajili ya kutaka kupata ufafanuzi wa sababu za kujiuzulu kwake, hakupokea simu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!