Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Katibu wa Bunge aficha sababu za Ghasia kujiuzuru
Habari za Siasa

Katibu wa Bunge aficha sababu za Ghasia kujiuzuru

Spread the love

HAWA Ghasia, Mbunge wa Mtwara Vijijini kupitia CCM, amejiuzulu uenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti leo tarehe 28 Agosti, 2018. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Vilevile, Jitu Soni, Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo pia amejiuzulu wadhifa huo.

Taarifa hizo zimethibitishwa na Stephen Kagaigai, Katibu wa Bunge alipozungumza na mtandao huu kwa njia ya simu.

Hata hivyo, Kagaigai hakutaka kuzungumzia sababu zilizopelekea viongozi hao kujiuzulu zaidi ya kusema kwamba Bunge lina taarifa za kujiuzulu kwao.

MwanaHALISI Online ilimtafuta Hawa Ghasia kwa njia ya simu kwa ajili ya kutaka kupata ufafanuzi wa sababu za kujiuzulu kwake, hakupokea simu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!