Thursday , 2 May 2024
KimataifaTangulizi

McCain afariki dunia

Spread the love

MPINZANI was Rais Mstaafu wa Marekani Barack Obama mwaka 2008 na seneta maarufu nchini Marekani, John McCain (81), amefariki dunia akiwa katika chumba chake cha mapumziko. Anaandika Mwandishi Wetu … (endelea).

McCain alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa saratani ya ubongo, amefariki katika chumba chake cha mapumziko mjini Sedona, Arizona, akiwa na familia yake.

Aidha, mwanasiasa huyo mkongwe aligundulika kuwa na ugonjwa huo hatari mwezi Julai mwaka 2017 ndipo alipoanza matibabu rasmi.

McCain aliwahi kuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya chama cha Republican mara mbili, na kuteuliwa kama mgombea rasmi mwaka wa 2008 ambapo alipambana na kushindwa na mgombea wa chama cha Demokratic, Barack Obama.

Hata hivyo, Rais wa Marekani, Donald Trump ameandika kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa maombi yake anayaelekeza kwa familia ya Seneta McCain ambaye aliwahi kulitumikia bunge la Marekani kwa miongo mitatu.

Pia aliwahi kuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya chama cha Republican mara mbili, na kuteuliwa kama mgombea rasmi mwaka wa 2008 ambapo alipambana na kushindwa na mgombea wa chama cha Demokratic, Barack Obama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!