Wednesday , 27 September 2023
Home Kitengo Michezo Messi amponza Rais wa Soka Palestina, afungiwa miaka 12
Michezo

Messi amponza Rais wa Soka Palestina, afungiwa miaka 12

Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA), kupitia kamati yake ya nidhamu imemfungia miaka 12, Rais wa Chama cha Soka cha Palestina, Jibfril Rajoub kutojihusisha na mchezo wa soka pamoja na faini kiasi cha Euro 15,826 baada ya kuagiza kuchomwa moto kwa jezi ya Messi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Adhabu hiyo imekuja baada baada ya rais wa chama soka cha Parestina kuaandikia barau Shirikisho la Soka Argentina akiwataka wasimchezeshe Lionel Messi katika mchezo wa kirafiki kati ya Argentina na Israel uliopangwa kuchezwa katika mji wa Jerusalem.

Na kama watakiuka tamko lake na Messi kuonekana mjini Jerusalem katika mchezo huo basi mashabiki wa soka nchini Palestina watafute jezi za nyota huyo popote pale nchini Palestina na wazichome moto.

Hata hivyo mchezo huo kati ya Argentina na Israel haukufanikiwa kucheza kutokana na kuhofia usalama wa wachezaji wao, kutokana na jambo hilo kuonekana kisiasa zaidi kutokana na nchi hizo mbili kuwa katika mvutano kwa miaka mingi sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

BiasharaMichezo

Piga pesa kupitia Derby ya London Kaskazini kwa kubadhiri na Meridianbet

Spread the love NAJUA umesikia na unazijua Derby nyingi kutoka jiji la London,...

error: Content is protected !!