Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kikwete, Cheyo kuwamwakilisha Rais Magufuli kuapishwa Mnangagwa
Habari za Siasa

Kikwete, Cheyo kuwamwakilisha Rais Magufuli kuapishwa Mnangagwa

Spread the love

DK. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, anatarajiwa kumwakilisha Rais John Magufuli katika sherehe za kuapishwa wa Emmerson Mnangagwa, Rais Mteule wa Jamhuri ya Zimbabwe zitakazofanyika Jumapili tarehe 26 Agosti, 2018 katika uwanja wa michezo wa Taifa Mjini Harare. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa kwa vyombo vya habari leo tarehe 25 Agosti, 2018 na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Taarifa hiyo ya Ikulu imeeleza kuwa, Rais Magufuli amemtuma Dk. Kikwete kumwakilisha ambapo atafuatana na Phillip Mangula, Makamu Mwenyekiti wa CCM na John Cheyo, Mwenyekiti wa chama cha UDP.

Rais Mnangagwa ataapishwa kesho kuongoza Zimbabwe baada ya kushinda katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 30 Julai, 2018 ikiwa anapokea kijiti kutoka kwa Robert Mugabe aliyekuwa Rais wa nchi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!