Thursday , 9 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Upandikizaji figo wazidi kufanikiwa Muhimbili
Afya

Upandikizaji figo wazidi kufanikiwa Muhimbili

Spread the love

IDADI ya wagonjwa waliofanyiwa huduma ya kupandikizaa figo katika hospitali ya Taifa Muhimbili imefikia 19 tangu kuanzishwa kwa huduma hiyo mwaka 2017. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa Huduma za Tiba katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dkt. Hedwiga Swai amesema kuwa utoaji wa huduma hiyo ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya awamu ya tano ya kupunguza rufaa za wagonjwa kwenda nje ya nchi kwa matibabu ambayo yalikuwa hayatilewi ndani ya nchi.

“Tayari wataalam wetu wa ndani hususan madaktari bingwa wamepata ujuzi wa kufanya upandikizaji wa figo kwa kiwango cha asilimia 75 huku asilimia 25 wakielekezwa na wataalam kutoka nje,” amesema.

Aidha Dkt. Swai amesema kuwa wanaahidi kufanya upandikizaji kwa angalau watu watano kwa mwezi ikiwa ni mpango wa muda mfupi kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu ambapo mpango wao wa kila siku ni kufanya upandikizaji kwa mgonjwa mmoja kila siku ambayo ni sawa na wagonjwa 20 kwa mwezi ambapo watakuwa wagonjwa 200 au 240 kwa mwaka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!