Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo TFF yateuwa waamuzi 82 kuchezesha Ligi Kuu
Michezo

TFF yateuwa waamuzi 82 kuchezesha Ligi Kuu

John Komba, mwamuzi wa Tanzania mwenye beji ya Fifa
Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), wamepitisha majina ya waamuzi 82, watakao chezesha michezo mbali mbali ya ligi kuu Tanzania bara katika msimu wa 2018/2019 inayotarajiwa kuanza kesho, huku waamuzi wa kati watakuwa 30, waamuzi wasaidizi 46, na waamuzi 6 waakiba. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Uteuzi huo umekuja baada ya kukamilika kwa mtihani wa kupima utimamu wa mwili kwa waamuzi hao uliofanyika mwezi huu Jijini Dar es Salaam ukisimamiwa na chama cha waamuzi nchini pamoja na baadhi ya watu kutoka ndani ya shirikisho la mpira wa miguu nchini.

Majina ya waamuzi waliopitishwa ni Athuman Selukala (Arusha), Erick Onoka (Arusha), Alex Magayi (Dar es Salaam), Elly Sasii (Dar es Salaam), Isihaka Mwalile (Dar es Salaam), Israel Nkongo (Dar es Salaam), Mbaraka Rashid (Dar es Salaam), Nadim Aloyce Leonard (Dar es Salaam) na Liston Hiyari (Dar es Salaam).

Wengine ni Florentina Zabron (Dodoma), Ally Simba (Geita), Amada Simba (Kagera),Jonesia Rukyaa (Kagera), Hussein Athumani (Katavi), Shomari Lawi (Kigoma), Alfred Vitares (Kilimanjaro), Jacob Adongo (Mara), Benedict Magai (Mbeya), Athumani Lazi, (Morogoro), Fikiri Yussuf (Morogoro), Martin Saanya (Morogoro), Abubakar Mturo (Mtwara), Daniel Warioba (Mwanza), Emmanuel Mwandembwa (Mwanza), Ludovick Charles (Mwanza), Ahmad Seif Mbaraka (Pwani), Nassoro Mwinchui (Pwani), Jimmy Fanuel (Shinyanga), Meshack Suda (Singida) na Hance Mabena wa Tanga.

1 Comment

  • Watu wengi tunahitaji koz za urefa,naomba usaidiz naanzeje,maana hatuoni matangazo,Hata kwenye blog za TFF hatuoni tukiuliza hatujibiw why so?vitu muhim ni vp,yaan ada,umri,elimi nk.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!