Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wabunge watatu Upinzani kutua CCM kabla Bunge kuanza
Habari za SiasaTangulizi

Wabunge watatu Upinzani kutua CCM kabla Bunge kuanza

Spread the love

WABUNGE watatu wa upinzani- wawili Chadema na mmoja Chama cha Wananchi (CUF), wako mbioni kuvikimbia vyama vyao na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Saed Kubenea … (endelea).

Habari kutoka kwa watu waliokaribu na wabunge hao na CCM zinasema, tayari mazungumzo ya kuwachukua wabunge hao tayari yamekamilika.

“Hawa wawili wataondoka wakati wowote. Tayari wameomba na kukubaliwa kujiunga na CCM. Huyu mmoja ameomba ashiriki mkutano huu wa Bunge ili aweke mambo yake, ikiwamo kuaga wabunge wenzake,” ameeleza kiongozi mmoja wa CCM kwa sharti la kutotajwa jina.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa huyo, wabunge wanaotaka kuondoka, wametaja sababu tofauti. Hakuzitaja.

MwanaHALISI Online inaendelea kufuatilia undani wa suala hilo na litaanika jina la kila mbunge na hata mpanga mkakati mwenyewe.

Kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja takribani mwezi mmoja tangu wabunge wengine wawili wa Chadema na mmoja wa CUF, kuvihama kwenye vyama vyao.

Wabunge walindoka Chadema, ni Mwita Mwaikabe Waitara (Ukonga) na Julius Kalanga (Monduli).

Kwa upande wa CUF, mbunge aliyehama na kujiunga na CCM, ni Zuber Mohammed Kuchauka (Liwale).

Aidha, kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja katika kipindi ambacho kumeongezeka wimbi la madiwani wa upinzani kuondoka kwenye vyama vyao na kujiunga na CCM.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, wabunge hao watatu, wameamua kuvihama vyama vyao kwa sababu zinazolingana.

“Wote watatu wanaondoka siyo kwa sababu wanaunga mkono juhudi, bali wanaondoka kutokana na matatizo wanayodai yapo kwenye vyama vyao,” ameeleza mmoja wa viongozi wa CCM aliyeshiriki mpango wa kuwachukua wabunge hao.

Anasema, mpango uliyopo mmoja wa wabunge anatarajiwa kuhama katika kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi mdogo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!