Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lugola awageukia Polisi wanaobambikia watu kesi
Habari za Siasa

Lugola awageukia Polisi wanaobambikia watu kesi

Kangi Lugola, Waziri wa mambo ya Ndani. Picha ndogo wakati akiapishwa
Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amehidi kufanya ziara za kushtukiza kwenye vituo vya polisi nchini ili kupambana na baadhi ya polisi wenye tabia ya kubambikizia kesi wananchi. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Waziri Lugola aliyasema hayo jana Agosti 9, 2018 wakati akihutubia kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wa Kijiji cha Kenkombyo wilayani Bunda.

Waziri Lugola alisema kitendo hicho kinaichafua wizara yake pamoja na serikali kwa ujumla, ambapo amesema polisi watakaobainika kufanya makosa hayo hata waonea huruma.

 “Nilishawaambia polisi na leo nawaaambia tena, nitakuwa nafanya ziara ya kushtukiza mara kwa mara katika vituo vya polisi, na hamjui saa wala siku lini nitakuja, hili nilisemalo sitanii kabisa, lazima nitapambana nanyi, hii ni serikali ya Awamu ya Tano inataka wananchi waishi kwa amani zaidi bila kua na hofu ya aina yoyote,” alisema Lugola.

Katika hatua nyingine, aliwataka wananchi waache tabia ya kufungua kesi polisi ili kuwakomoa watu wenye chuki nao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!