Saturday , 2 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge wa Chadema awamwaga Polisi
Habari za Siasa

Mbunge wa Chadema awamwaga Polisi

Pascal Haonga, Mbunge wa Mbozi (mwenye kombati nyeusi) akiwa na wadau wengine wakishangilia
Spread the love

MBUNGE wa jimbo la Mbozi mkoani Songwe kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Pascal Haonga na wenzake wameshinda kesi iliyokuwa inawakabili katika Mahakama ya Wilaya ya Mbozi, baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha makosa dhidi ya watuhumiwa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Haonga na wengine Katibu wake Wilfred Mwalusamba na Mashaka Mwampashi walikuwa wakikabiliwa na makosa ya kuvuruga mkutano wa uchaguzi wa baraza la mji mdogo wa Mlowo kosa la pili na la tatu kuwazuia askari kutekeleza majukumu yao makosa hayo wanadaiwa kuyatenda tarehe 28 Agosti, mwaka huu.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mfawidhi Nemes Chami alisema katika mashtaka yote matatu yalikuwa yanawakabili, hakuna hata sehemu moja upande wa mashtaka uliothibitisha.

“Hakuna mahali walipoonesha kwamba washtakiwa hawa waliwazuia askari kutekeleza majukumu yao na hakuna mahali walipo thibitisha kwamba washtakiwa walilazimisha kurudi ukumbini baada ya kutolewa nje” Alisema Chami.

Baada ya kusoma hukumu hiyo hakimu huyo alisema kuwa kama kuna upande ambao haujarizika na hukumu hiyo una haki ya kukata rufaa ndani ya muda.

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia kuzindua programu ya nishati safi ya kupikia kwa wanawake Afrika

Spread the loveRais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua programu ya...

Habari za Siasa

AG aiagiza kamati ya maadili kuwashughulikia mawakili wanaokiuka maadili

Spread the loveMWANASHERIA Mkuu wa Serikali (AG), Dk. Eliezer Feleshi, ameagiza Kamati...

Habari za Siasa

Jaji avunja ukimya sakata la Mpoki kusimamishwa uwakili

Spread the loveJAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma, amekitaka Chama cha...

Habari za Siasa

Sheikh Ponda ataka mwarobaini changamoto uchaguzi 2020

Spread the loveKATIBU Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa...

error: Content is protected !!