WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amehidi kufanya ziara za kushtukiza kwenye vituo vya polisi nchini ili kupambana na baadhi ya polisi wenye tabia ya kubambikizia kesi wananchi. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Waziri Lugola aliyasema hayo jana Agosti 9, 2018 wakati akihutubia kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wa Kijiji cha Kenkombyo wilayani Bunda.
Waziri Lugola alisema kitendo hicho kinaichafua wizara yake pamoja na serikali kwa ujumla, ambapo amesema polisi watakaobainika kufanya makosa hayo hata waonea huruma.
“Nilishawaambia polisi na leo nawaaambia tena, nitakuwa nafanya ziara ya kushtukiza mara kwa mara katika vituo vya polisi, na hamjui saa wala siku lini nitakuja, hili nilisemalo sitanii kabisa, lazima nitapambana nanyi, hii ni serikali ya Awamu ya Tano inataka wananchi waishi kwa amani zaidi bila kua na hofu ya aina yoyote,” alisema Lugola.
Katika hatua nyingine, aliwataka wananchi waache tabia ya kufungua kesi polisi ili kuwakomoa watu wenye chuki nao.
Leave a comment