Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lugola awageukia Polisi wanaobambikia watu kesi
Habari za Siasa

Lugola awageukia Polisi wanaobambikia watu kesi

Kangi Lugola, Waziri wa mambo ya Ndani. Picha ndogo wakati akiapishwa
Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amehidi kufanya ziara za kushtukiza kwenye vituo vya polisi nchini ili kupambana na baadhi ya polisi wenye tabia ya kubambikizia kesi wananchi. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Waziri Lugola aliyasema hayo jana Agosti 9, 2018 wakati akihutubia kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wa Kijiji cha Kenkombyo wilayani Bunda.

Waziri Lugola alisema kitendo hicho kinaichafua wizara yake pamoja na serikali kwa ujumla, ambapo amesema polisi watakaobainika kufanya makosa hayo hata waonea huruma.

 “Nilishawaambia polisi na leo nawaaambia tena, nitakuwa nafanya ziara ya kushtukiza mara kwa mara katika vituo vya polisi, na hamjui saa wala siku lini nitakuja, hili nilisemalo sitanii kabisa, lazima nitapambana nanyi, hii ni serikali ya Awamu ya Tano inataka wananchi waishi kwa amani zaidi bila kua na hofu ya aina yoyote,” alisema Lugola.

Katika hatua nyingine, aliwataka wananchi waache tabia ya kufungua kesi polisi ili kuwakomoa watu wenye chuki nao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!