Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa TEF, TFF wapinga wanahabari kushambuliwa
Habari za SiasaMichezo

TEF, TFF wapinga wanahabari kushambuliwa

Spread the love

JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF) limelaani kitendo cha Jeshi la Polisi kumfungulia Mwanahabari wa gazeti la Tanzania Daima, Sitta Tuma mashitaka ya kuandamana bila kibali. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Tamko la TEF lilitolewa hapo jana Agosti 9, 2018 na Kaimu Mwenyekiti wake, Deodatus Balile ambapo alisema mwanahabari huyo alikuwa kazini akitekeleza wajibu wake wa kukusanya habari.

Tuma alikamatwa Agosti 8 mwaka huu pamoja na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko na wafuasi  18 wa chama cha Chadema wakiwa kwenye mkutano wa kampeni ya mgombea udiwani wa chama hicho Kata ya Turwa.

Wakati TEF likipinga kukamatwa kwa mwanahabari Tuma, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania  (TFF) jana lilitoa tamko la kulaani tukio la shambulio lililodaiwa kufanywa na polisi kwa mwandishi wa habari za Michezo, Sillas Mbise lililotokea katika mchezo wa kirafiki kati ya Simba na Asante Kotoko kutoka Ghana uliofanyika  uwanja wa Taifa juzi Agosti 8, 2018.

Kufuatia kadhia hiyo, TFF imesema imekutana na viongozi wa Chama cha waandishi wa habari za michezo nchini TASWA na kujadiliana kuhusu tukio hilo na hatua stahiki zitachukuliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

error: Content is protected !!