Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri wa Madini afunga mgodi Pwani
Habari za Siasa

Waziri wa Madini afunga mgodi Pwani

Spread the love

SERIKALI imesimamisha shughuli za mgodi unaochimbwa madini ya Kaolin unaomilikiwa na kampuni ya RAK Kaolin kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wa uendeshaji wake na biashara ya madini hayo viwandani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Agizo hilo lilitolewa jana na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uchimbaji madini ya ujenzi Julai 25,2018.

Waziri Nyongo alitoa agizo hilo baada ya kutoridhishwa na shughuli za mgodi huo uliopo katika Kijiji cha Kimani wilayani Kisarawe mkoani Pwani, ikiwemo umiliki wa ardhi, leseni ya mgodi, uchimbaji pamoja na biashara ya madini hayo viwandani.

Waziri Nyongo alisema shughuli za uchimbaji na biashara ya madini katika mgodi huo hazioneshi wazi taratibu za ulipaji serikalini, mrabaha na tozo mbalimbali zilizowekwa kwa mujibu wa sheria.

Aidha, alimtaka mmiliki wa leseni ya mgodi huo kuwasilisha wizara ya madini nakala ya mkataba walioingia kati yake na wachimbaji wa madini ya Kaolin katika mgodi huo, na namna ambavyo aliweza kumiliki eneo husika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!