Friday , 2 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri wa Madini afunga mgodi Pwani
Habari za Siasa

Waziri wa Madini afunga mgodi Pwani

Spread the love

SERIKALI imesimamisha shughuli za mgodi unaochimbwa madini ya Kaolin unaomilikiwa na kampuni ya RAK Kaolin kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wa uendeshaji wake na biashara ya madini hayo viwandani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Agizo hilo lilitolewa jana na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uchimbaji madini ya ujenzi Julai 25,2018.

Waziri Nyongo alitoa agizo hilo baada ya kutoridhishwa na shughuli za mgodi huo uliopo katika Kijiji cha Kimani wilayani Kisarawe mkoani Pwani, ikiwemo umiliki wa ardhi, leseni ya mgodi, uchimbaji pamoja na biashara ya madini hayo viwandani.

Waziri Nyongo alisema shughuli za uchimbaji na biashara ya madini katika mgodi huo hazioneshi wazi taratibu za ulipaji serikalini, mrabaha na tozo mbalimbali zilizowekwa kwa mujibu wa sheria.

Aidha, alimtaka mmiliki wa leseni ya mgodi huo kuwasilisha wizara ya madini nakala ya mkataba walioingia kati yake na wachimbaji wa madini ya Kaolin katika mgodi huo, na namna ambavyo aliweza kumiliki eneo husika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!