KARNE ya 21 inatarajiwa kushuhudia tukio kubwa na la muda mrefu la kupatwa kwa mwezi Ijumaa ya Julai 27, 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Ni tukio kubwa kutokana na kupatwa huko kutachukua muda mrefu zaidi tofauti na matukio yaliyowahi kutokea awali.
Kwa mujibu wa mtandao wa bbc, Shirika la Usimamizi wa Anga za Juu (NASA) limeeleza kuwa, tukio hilo litakuwa la muda mrefu zaidi katika karne hii ya 21.
Tukio hilo linatarajiwa kudumu kwa muda wa dakika 103 ambapo katika awamu tofauti kupatwa huko kwa mwezi kutafanyika kwa saa tatu na dakika 55.
Kupatwa kwa mwezi hutokea wakati jua, dunia na mwezi zinapokua kwenye mstari mmoja kwa maana ya kuwa dunia inakuwa katikati ya jua na mwezi hatua inayoziba mwanga wa jua.
Kupatwa huko hutokea wakati mwezi unapoingia katika kivuli cha dunia.
BBC imeeleza kuwa, kupatwa huko kwa mwezi Julai 27 kutaonekana Ulaya, Afrika, Mashariki ya Kati, katikati mwa Asia na Australia ikiwa ni maeneo yote isipokuwa Kaskazini mwa Marekani.
Eneo zuri la kulitazama tukio hilo ni eneo nusu ya Mashariki mwa Afrika, Mashariki ya Kati na katikati mwa bara Asia. Tukio hilo halitaonekana katika maeneo ya kati na Marekani Kaskazini.
Kusini mwa Marekani unaweza kuonekana kiasi katika maeneo ya mashariki hususani miji ya Buenos Aires, Montevideo, Sao Paulo na Rio de Janeiro.
Katika miji mingine ya karibu utaonekana wakati mwezi utakapokuwa ukiondoka katika eneo hilo.
Leave a comment