Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Tukio kubwa kuikumba dunia kesho (Julai 27)
Kimataifa

Tukio kubwa kuikumba dunia kesho (Julai 27)

Spread the love

KARNE ya 21 inatarajiwa kushuhudia tukio kubwa na la muda mrefu la kupatwa kwa mwezi Ijumaa ya Julai 27, 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ni tukio kubwa kutokana na kupatwa huko kutachukua muda mrefu zaidi tofauti na matukio yaliyowahi kutokea awali. 

Kwa mujibu wa mtandao wa bbc, Shirika la Usimamizi wa Anga za Juu (NASA) limeeleza kuwa, tukio hilo litakuwa la muda mrefu zaidi katika karne hii ya 21.

Tukio hilo linatarajiwa kudumu kwa muda wa dakika 103 ambapo katika awamu tofauti kupatwa huko kwa mwezi kutafanyika kwa saa tatu na dakika 55.

Kupatwa kwa mwezi hutokea wakati jua, dunia na mwezi zinapokua kwenye mstari mmoja kwa maana ya kuwa dunia inakuwa katikati ya jua na mwezi hatua inayoziba mwanga wa jua.

Kupatwa huko hutokea wakati mwezi unapoingia katika kivuli cha dunia.

BBC imeeleza kuwa, kupatwa huko kwa mwezi Julai 27 kutaonekana Ulaya, Afrika, Mashariki ya Kati, katikati mwa Asia na Australia ikiwa ni maeneo yote isipokuwa Kaskazini mwa Marekani.

Eneo zuri la kulitazama tukio hilo ni eneo nusu ya Mashariki mwa Afrika, Mashariki ya Kati na katikati mwa bara Asia. Tukio hilo halitaonekana katika maeneo ya kati na Marekani Kaskazini.

Kusini mwa Marekani unaweza kuonekana kiasi katika maeneo ya mashariki hususani miji ya Buenos Aires, Montevideo, Sao Paulo na Rio de Janeiro.

Katika miji mingine ya karibu utaonekana wakati mwezi utakapokuwa ukiondoka katika eneo hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!