MANGE Kimambi, raia wa Tanzania anayeishi Marekani, ni miongoni mwa wanawake wanaharakati wa kisiasa wanaotajwa kwenye orodha ya kugombea tuzo ya mwanamke mhamasishaji zaidi kisiasa Afrika. Anaandika Mwandishi Wetu…(endelea).
Tuzo hiyo imeandaliwa na Shirika la Black Entertainment Film Fashion Television and Art (BEFFTA) –Burudani, Filamu, Mitindo, Televisheni ya Watu Aweusi.
Taarifa za kuwania tuzo hizo zilitolewa na shirika hilo la BFFTA kupitia ukurasa wao unaopatikana kwenye mtandao wa kijamii wa instagram.
Shirika hilo lengo lake kuu ni kuangaza maslahi ya watu weusi katika nchi za Uingereza, Canada, Marekani, Carribbean na nchi za bara la Afrika.
Wengine waliojuimushwa katika kipengele hicho ni Elie Johson Sirleaf wa Liberia, Joice Majuru kutoka Zimbabwe, Diane Shima Rwigara raia wa Rwanda, Mbali Ntuli kutoka South Afrika na Alengot Oromait kutoka nchini Uganda.
Mange amejipatia umaarufu katika mitandao ya kijamii hasa instagram kutokana jumbe zake za ukosoaji kwa viongozi wa serikali na hata viongozi wa dini nchini Tanzania.
Pia aliongeza ‘presha’ zaidi Tanzania kutokana na kutumia mitandao ya kijamii kuhamasisha maandamano aliyopanga kufanyika Aprili 26 mwaka huu.
Hatua hiyo hiyo iliwalazimu viongozi mbalimbali Tanzania kujitokeza na kupinga maandamano hayo yaliyoonekana kushika kasi kupitia mitandao hiyo.
Leave a comment