Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watakaobadili matumizi ya kanisa kulaaniwa
Habari Mchanganyiko

Watakaobadili matumizi ya kanisa kulaaniwa

Spread the love

WAUMINI wa Kanisa la Mama Maria Mkuu wa Kanisa la Kigurunyembe Manispaa ya Morogoro mkoani hapo wameaswa kutobadili matumizi ya kanisa hilo na na endapo watabadilisha matumizi watalaaniwa. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Askofu wa Jimbo Kuu Katoliki jijini Dar es Salaam, Mwadhama Polycard Kardinaly Pengo wakati akiweka wakfu baada ya kuzindua kanisa hilo jipya lilijengwa kwa thamani ya shilingi mil 860.

Kardinary Pengo alisema kuwa kanisa ni hekalu la Mungu ambapo ni mahali patakatifu panapotakiwa kuheshimiwa kwa utakatifu wake sambamba na utakatifu wa waumini wenyewe.

“Kanisa hili ni mahali patakatifu kuanzia leo na mkibadilisha mawazo mkafanya kuwa mahali pa matumizi mengine na lisiwe kanisa hata na Askofu wenu Mkude, hapo mtakuwa mmelaaniwa, nitawashitaki” alisema Kardinary Pengo.

Alisema uzuri na ukubwa na uzuri wa jengo hilo ungefanya watu wengine wasio na mioyo ya utakatifu kulibadilisha matumizi na kuwa kumbi ya starehe na kwamba utakatifu wao ndio umejidhihirisha kulifanya kuwa kanisa.

Naye Mkuu Mkoa wa Morogoro Dk. Kebwe Steven Kebwe aliwaagiza waumini wa kanisa hilo kuhakikisha wanalitunza kanisa hilo ili liweze kudumu zaidi ya miaka 100.

Aidha Dk. Kebwe alisema kuwa huduma za kijamii zimekuwa zikibebwa kwa sehemu kubwa chini ya dini zote ikiwemo elimu, maji, na malezi ya kiroho sambamba na amani ya nchi.

Dk. Kebwe alisema katika kuonesha dhamira hiyo ya kuanzisha huduma za kijamii anatoa shilingi laki tano kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Paroko hali ambayo ilichangia kupatikana zaidi ya sh Mil 1.75 na mifuko 100 ya saruji ambayo iliahidiwa kutolewa na Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete.

Aidha, Kikwete alisema familia yao haitaweza kuisahau dini ya Kikristo hasa Roma kwa kuweza kuwa njia ya kuinuka kielimu na kimaisha kufuatia ndugu wengi kupata elimu katika shule za kimisionari.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!