Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watakaobadili matumizi ya kanisa kulaaniwa
Habari Mchanganyiko

Watakaobadili matumizi ya kanisa kulaaniwa

Spread the love

WAUMINI wa Kanisa la Mama Maria Mkuu wa Kanisa la Kigurunyembe Manispaa ya Morogoro mkoani hapo wameaswa kutobadili matumizi ya kanisa hilo na na endapo watabadilisha matumizi watalaaniwa. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Askofu wa Jimbo Kuu Katoliki jijini Dar es Salaam, Mwadhama Polycard Kardinaly Pengo wakati akiweka wakfu baada ya kuzindua kanisa hilo jipya lilijengwa kwa thamani ya shilingi mil 860.

Kardinary Pengo alisema kuwa kanisa ni hekalu la Mungu ambapo ni mahali patakatifu panapotakiwa kuheshimiwa kwa utakatifu wake sambamba na utakatifu wa waumini wenyewe.

“Kanisa hili ni mahali patakatifu kuanzia leo na mkibadilisha mawazo mkafanya kuwa mahali pa matumizi mengine na lisiwe kanisa hata na Askofu wenu Mkude, hapo mtakuwa mmelaaniwa, nitawashitaki” alisema Kardinary Pengo.

Alisema uzuri na ukubwa na uzuri wa jengo hilo ungefanya watu wengine wasio na mioyo ya utakatifu kulibadilisha matumizi na kuwa kumbi ya starehe na kwamba utakatifu wao ndio umejidhihirisha kulifanya kuwa kanisa.

Naye Mkuu Mkoa wa Morogoro Dk. Kebwe Steven Kebwe aliwaagiza waumini wa kanisa hilo kuhakikisha wanalitunza kanisa hilo ili liweze kudumu zaidi ya miaka 100.

Aidha Dk. Kebwe alisema kuwa huduma za kijamii zimekuwa zikibebwa kwa sehemu kubwa chini ya dini zote ikiwemo elimu, maji, na malezi ya kiroho sambamba na amani ya nchi.

Dk. Kebwe alisema katika kuonesha dhamira hiyo ya kuanzisha huduma za kijamii anatoa shilingi laki tano kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Paroko hali ambayo ilichangia kupatikana zaidi ya sh Mil 1.75 na mifuko 100 ya saruji ambayo iliahidiwa kutolewa na Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete.

Aidha, Kikwete alisema familia yao haitaweza kuisahau dini ya Kikristo hasa Roma kwa kuweza kuwa njia ya kuinuka kielimu na kimaisha kufuatia ndugu wengi kupata elimu katika shule za kimisionari.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!