Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mil 46 zatengwa kusimamia misitu
Habari Mchanganyiko

Mil 46 zatengwa kusimamia misitu

Spread the love

JUMLA ya shilingi mil 46 zimetengwa na Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa mkoani hapa kwa mwaka wa fedha 2018/19 kwa ajili ya Usimamizi Shirikishi wa Misitu ya Jamii (CBFM) katika vijiji  vitatu wilayani humo. Anaripoti Christina Haule, Kilosa … (endelea).

Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Idara ya Maliasili, Ardhi na Misitu wilaya ya Kilosa, Ibrahim Ndembo wakati akizungumza na waandishi wa habari wilayani humo.

Ndembo amesema halmashauri imekubali kutenga fedha hizo ili kuweza kuendeleza jitihada ambazo zimefanywa na Mradi wa Kuleta Mageuzi katika Sekta ya Mkaa Tanzania (TTCS) katika vijiji 20 vya wilayani hapo.

Amesema halmashauri katika kutekeleza dhana ya CBFM iliyoanza kutekelezwa na Mradi wa CBFM  katika vijiji hivyo vya New Mamboya, Inyunywe na Nyangala kutasaidia kuokoa misitu ambayo inaharibiwa kwa wingi na wavunaji misitu wasiofuata usimamizi wa shirikishi wa misitu.

Mkuu huyo wa idara amesema lengo ni kutekeleza dhana ya CBFM katika vijiji vitano kila mwaka wa fedha ila kutokana na uhaba wa fedha wataanza na vijiji hivyo vitatu.

Ndembo amesema matarajio yao ni kupitia Baraza la Madiwani katika mwaka wa fedha 2019/2020 watatenga fedha nyingine kwa ajili vijiji vingine vya Kaskazini hasa Dumila ili kufikia vijiji 20 mwaka 2021.

Mkuu huyo wa idara amesema Kilosa ina vijiji 139 na vijiji ambavyo vinatekeleza CBFM ni 20 na vyote vipo Kusini.

Amesema watatumia wana vijiji kutoka Kusini kutoa elimu ya CBFM na mkaa endelevu katika vijiji vipya vya mradi, wanachofanya ni kusimamia Sheria na Sera ya Misitu ambayo inahitaji kuwepo kwa CBFM.

Akizungumzia CBFM, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kilosa Hassan Mkopi amesema madiwani wote wameridhia utengaji wa fedha hizo kwa ajili ya CBFM hivyo kuwataka watendaji kutekeleza kwa ufanisi.

Mkopi amesema mradi wa TTCS umekuwa mkombozi mkubwa katika utunzaji mazingira na uchumi wa wana vijiji wao hivyo ni lazima uwe endelevu.

Naye Kaimu Meneja wa Mradi wa TTCS, Simon Lugazo amesema mradi huo unatarajia kufikia mwisho hivyo wamelazimika kuwaita wadau wa Serikali na madiwani ili kujua wamejipangaje kuendeleza mradi huo.

Amesema mradi huo unaotekelezwa na Shirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania (TFCG), Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania (Mjumita) na Shirika la Kuendeleza Nishati Asilia Tanzania (TaTEDO) kupitia Ufadhili wa Shirika la Maendeleo na Ushirikiano la Uswis (SDC), umefanikiwa kuokoa uharibifu wa misitu kwa zaidi ya asilimia moja kwa miaka michache ya uwepo wake.

Lugazo amesema mradi wa TTCS umesaidia usimamizi misitu shirikishi, utawala bora na sheria huku pia zaidi Sh.Mil 800 zikikusanywa wilayani Kilosa katika mauzo ya maliasili za misitu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!