Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa IGP, DCI ‘wamkimbia’ Nondo mahakamani Dar
Habari za SiasaTangulizi

IGP, DCI ‘wamkimbia’ Nondo mahakamani Dar

Mawakili wa Abdul Nondo wakiwa Mahakama Kuu muda mchache baada ya kesi yao
Spread the love

WAKATI Mwenyekiti wa Mtandao wa Wananfunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo akipandishwa kizimbani leo asubuhi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam nayo imeanza kusikiliza kesi ya Nondo dhidi ya Serikali, akidai haki ya uwakilishi pamoja na dhamana. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mawakili wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), na wale wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) wakiongozwa na Mpoki Mpare na Jebra Kambole wamefika mbele ya Jaji Rehema Semeji na kuwasilisha mashtaka dhidi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Mwanasheria Mkuu (AG) na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP).

Katika kesi hiyo namba 49 ya mwaka 2018, mawakili hao wameiomba mahakama kuiamuru serikali kutoa dhamana na kuruhusu haki ya uwakilishi kwa mteja wao Nondo.

Amesema, “Maombi haya yalifunguliwa dhidi ya DCI, IGP, AG tukiomba mahakama kutoa amri ya kuletwa mahakamani kwa mwanafunzi Nondo au kumuachia kwa dhamana kwani ameshikiliwa na polisi kwa muda mrefu bila sababu za msingi kutolewa”

Jaji Sameja ameutaka upande wa Jamhuri kujibu hoja za utetezi Machi 26, 2018.

Jaji Semeji amesikilia maombi hayo na kueleza kuwa shauri hilo litaendelea kusikilizwa Aprili 4 Mwaka huu.

Nondo ambaye ni Mwanafunzi wa Mwaka wa tatu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kitivo Sayansi ya Siasa na Utawala amefikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa.

Na kusomewa mashtaka mawili na wakili wa serikali Abeid Mwandalamo mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, John Mpitanjia.

Mwandalamo Amedai kuwa kosa la kwanza ni kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni Machi 7, 2018 akiwa eneo la Ubungo Dar es Salaam na kuzisambaza kupitia mtandao wa kijamii wa Whatsapp kwamba yupo hatarini.

Katika shtaka la pili, ni kutoa taarifa za uongo kwa mtumishi wa umma Mafinga alipokuwa anatoa taarifa kwa askari kwenye Kituo cha Polisi Mafinga kwa kusema kuwa alitekwa na watu wasiojulikana Dar es Salaam na kupelekwa kiwanda cha Pareto Mafinga. Hata hivyo, Nondo alikana mashtaka hayo.

Mwanadalamo amedai ushahidi bado haujakamilika hivyo wanaomba siku chache, kwa kipindi watakachokuwa wanafanya upelelezi mtuhumiwa asipewe dhamana.

Amedai kuwa kwa sababu bado wanafanya upelelezi kwa rafiki wake wa karibu, kama atapewa dhamana anaweza kuingilia na kuharibu upelelezi huo.

Hata hivyo Wakili wa utetezi, Chance Luwoga amesema mashtaka aliyosomewa Nondo yanaruhusu kupewa dhamana hivyo hakuna sababu za msingi za kuzuiliwa kwa dhamana ya mteja wake.

Hakimu Mpitanjia amesema kuwa Mahakama hiyo itatoa uamuzi juu ya dhamanda ya mshukiwa huyo tarehe 26 Machi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!